Jumanne, 31 Desemba 2019
FURAHA NA SHANGWE 2020
Jumamosi, 28 Desemba 2019
Tumkumbuke mungu
Kumbukumbu la Torati 13:1-5
Kumbukumbu la Torati
13 “Ikiwa nabii au mtu anayebashiri kupitia ndoto atatokea miongoni mwenu na kuwapa ishara au dalili ya ajabu, 2 kisha ishara au dalili hiyo aliyowaambia itimie wakati anaposema, ‘Acheni tuifuate miungu mingine, miungu msiyoijua, na acheni tuiabudu,’ 3 hampaswi kusikiliza maneno ya nabii huyo au mwotaji huyo wa ndoto,+ kwa sababu Yehova Mungu wenu anawajaribu+ ili ajue ikiwa mnampenda Yehova Mungu wenu kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote.+ 4 Mnapaswa kumfuata Yehova Mungu wenu, mnapaswa kumwogopa yeye, mnapaswa kushika amri zake, mnapaswa kuisikiliza sauti yake; yeye ndiye mnayepaswa kumtumikia, nanyi mnapaswa kushikamana naye kabisa.+ 5 Lakini nabii huyo au mwotaji huyo wa ndoto anapaswa kuuawa,+ kwa sababu aliwachochea mmwasi Yehova Mungu wenu—aliyewatoa nchini Misri na kuwakomboa kutoka katika nyumba ya utumwa—ili mtoke katika njia ambayo Yehova Mungu wenu amewaamuru mtembee. Nanyi lazima mwondoe kilicho kiovu kutoka miongoni mwenu.+
6 “Ikiwa ndugu yako, mwana wa mama yako, au mwana wako au binti yako au mke wako mpendwa au rafiki yako wa karibu sana* atajaribu kukushawishi kwa siri, akisema, ‘Twende tukaabudu miungu mingine,’+ miungu ambayo wewe wala mababu zako hamwijui, 7 kutoka miongoni mwa miungu ya mataifa yanayowazunguka, yaliyo karibu nanyi au mbali nanyi, kutoka mwisho mmoja wa nchi mpaka mwisho mwingine wa nchi, 8 usikubali ushawishi wake wala kumsikiliza,+ wala usimsikitikie wala kumhurumia wala kumlinda; 9 badala yake, ni lazima umuue.+ Mkono wako unapaswa kuwa wa kwanza kumuua, kisha mikono ya watu wote itafuata.+ 10 Nawe lazima umuue kwa kumpiga mawe,+ kwa sababu alijaribu kukugeuza umwache Yehova Mungu wako, aliyekutoa nchini Misri, kutoka katika nyumba ya utumwa. 11 Hivyo, Waisraeli wote watasikia na kuogopa, na kamwe hawatafanya tena jambo lolote baya kama hilo miongoni mwenu.+
12 “Ikiwa mtasikia ikisemwa hivi katika mojawapo ya majiji yenu ambayo Yehova Mungu wenu anawapa mkae humo: 13 ‘Watu wasiofaa kitu wametokea miongoni mwenu ili kuwapotosha wakaaji wa jiji lao, wakisema, “Twendeni tukaabudu miungu mingine,” miungu ambayo hamwijui,’ 14 mnapaswa kupeleleza jambo hilo, kufanya uchunguzi kamili na kuuliza kwa makini;+ na ikithibitishwa ni kweli kwamba jambo hilo lenye kuchukiza limefanywa miongoni mwenu, 15 ni lazima muwaangamize kwa upanga wakaaji wa jiji hilo.+ Mtawaangamiza+ kwa upanga watu wa jiji hilo pamoja na kila kitu kilichomo, kutia ndani mifugo yao. 16 Kisha mtakusanya nyara zote za jiji hilo katikati ya uwanja wa jiji na kuliteketeza jiji hilo kwa moto, na nyara hizo zitakuwa dhabihu nzima ya kuteketezwa kwa Yehova Mungu wenu. Nalo litabaki rundo la magofu milele. Halipaswi kamwe kujengwa tena. 17 Mikono yenu haipaswi kuchukua kitu chochote kinachopaswa kuharibiwa,*+ ili Yehova aache hasira yake kali na kuwaonyesha rehema na huruma na kuwafanya mwongezeke, kama alivyowaapia mababu zenu.+ 18 Kwa maana mnapaswa kumtii* Yehova Mungu wenu kwa kushika amri zake zote ambazo ninawaamuru leo, na hivyo kufanya yaliyo sawa machoni pa Yehova Mungu wenu.+
Kiswahili Mapendezi
Copyright © 2019 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania Masharti ya Utumiaji Sera ya Faragha JW.ORG Ingia
Ijumaa, 27 Desemba 2019
Neno la mungu
wp20 Na. 1 uku. 6
Audio Player
00:00
Biblia—Chanzo Kinachotegemeka cha Kweli
Historia inaonyesha kwamba kwa miaka mingi watu wa jamii mbalimbali wameiona Biblia kuwa chanzo kinachotegemeka cha kupata kweli. Leo, watu wengi wanafuata mafundisho yake. Hata hivyo, wengine huiona Biblia kuwa kitabu kisicho na manufaa au cha uwongo. Wewe una maoni gani? Je, mafundisho ya kweli yanaweza kupatikana katika Biblia?
KWA NINI UNAWEZA KUITUMAINI BIBLIA
Una msingi gani wa kuamini kwamba Biblia ina mafundisho ya kweli? Fikiria mfano huu: Ikiwa una rafiki ambaye sikuzote anakwambia ukweli, bila shaka utamwamini. Je, Biblia ni kama rafiki huyo mwenye kutegemeka ambaye husema kweli nyakati zote? Acheni tuchunguze mifano kadhaa.
Waandikaji Wanyoofu
Waandikaji wa Biblia walikuwa wanyoofu sana na mara nyingi waliandika kuhusu makosa na udhaifu wao. Kwa mfano, nabii Yona aliandika jinsi alivyokosa kutii maagizo ya Mungu. (Yona 1:1-3) Kwa kweli, alihitimisha uandishi wa kitabu chake kwa kutaja jinsi Mungu alivyomrekebisha, hata hivyo hakujielekezea uangalifu kwa kueleza jinsi alivyobadili mtazamo wake. (Yona 4:1, 4, 10, 11) Unyoofu wa waandikaji wote wa Biblia unaonyesha kwamba walihangaikia sana kweli.
Ushauri Unaotegemeka
Je, ushauri wa Biblia kuhusu mambo ya kawaida maishani unategemeka? Bila shaka. Kwa mfano, fikiria kile ambacho Biblia inasema kuhusu jinsi ya kudumisha uhusiano mzuri na wengine. Inasema hivi: “Basi, mambo yote mnayotaka watu wawatendee ninyi, lazima ninyi pia mwatendee vivyo hivyo.” (Mathayo 7:12) “Jibu la upole hutuliza hasira, lakini neno kali huchochea hasira.” (Methali 15:1) Naam, mafundisho ya Biblia yana manufaa leo kama ilivyokuwa yalipoandikwa.
Ni Sahihi Kihistoria
Vitu vya kale vilivyochimbuliwa vinathibitisha usahihi wa matukio yanayotajwa katika Biblia, kutia ndani watu na maeneo yanayosimuliwa. Kwa mfano, fikiria uthibitisho mdogo uliotolewa. Biblia inasema kwamba katika siku za Nehemia, Watiro (Wafoinike kutoka Tiro) walioishi Yerusalemu “walikuwa wakileta samaki na bidhaa za kila aina.”—Ne[hemia] 13:16.
Je, kuna uthibitisho wowote unaounga mkono mstari huo wa Biblia? Ndiyo. Wachimbuzi wa vitu vya kale wamevumbua vitu vilivyotumiwa na Wafoinike nchini Israeli, ikithibitisha kwamba mataifa hayo mawili yalifanya biashara. Kwa kuongezea, mabaki ya samaki wanaopatikana katika eneo la Mediterania yamepatikana huko Yerusalemu. Wachimbuzi wa vitu vya kale wanaamini kwamba samaki hao waliletwa na wafanyabiashara kutoka maeneo ya mbali. Baada ya kuchunguza uthibitisho huo, msomi mmoja alisema hivi: “Maneno yaliyo kwenye Nehemia] 13:16 kwamba Watiro walifanya biashara ya kuuza samaki huko Yerusalemu ni ya kweli.”
Ni Sahihi Kisayansi
Biblia ni kitabu hasa cha kidini na cha kihistoria. Hata hivyo, inapozungumzia mambo ya sayansi, inapatana kabisa na mambo yaliyothibitishwa kisayansi. Hebu tuchunguze mfano mmoja.
Karibu miaka 3,500 iliyopita, Biblia ilitaja kwamba dunia imening’inizwa “mahali pasipo na kitu.” (Ayubu 26:7) Maneno hayo ni tofauti na hadithi zilizosema kwamba dunia inaelea juu ya maji au imebebwa na kobe mkubwa sana. Miaka 1,100 hivi baada ya kitabu cha Ayubu kuandikwa, watu waliendelea kuamini kwamba dunia haiwezi kuning’inia yenyewe; lazima iwe imeshikiliwa na kitu fulani. Watu waliendelea kuwa na maoni hayo hadi miaka mia tatu tu iliyopita, yaani, mwaka wa 1687 wakati Isaac Newton alipoandika utafiti wake kuhusu nguvu za uvutano na kuonyesha kwamba dunia ni duara na inaning’inia yenyewe kwa sababu ya nguvu zisizoonekana. Utafiti huo wa kisayansi ulithibitisha maneno yaliyoandikwa zaidi ya miaka 3,000 iliyopita!
Unabii Wake ni Sahihi
Unabii mwingi ulio katika Biblia ni sahihi kadiri gani? Fikiria mfano mmoja: Unabii wa Isaya kuhusu kuanguka kwa jiji la Babiloni.
Unabii: Katika karne ya nane K.W.K., Isaya, mwandikaji wa Biblia alitangaza kwamba jiji la Babiloni—ambalo baada ya muda lingekuwa jiji kuu la milki yenye nguvu zaidi ulimwenguni—lingeanguka na halingekaliwa tena. (Isaya 13:17-20) Isaya hata alitaja jina la kiongozi ambaye angetimiza unabii huo, yaani, Koreshi. Pia alitaja mbinu ambayo Koreshi angetumia, kwamba ‘angekausha’ mito. Na alitabiri kwamba malango ya jiji yangeachwa yakiwa wazi.—Isaya 44:27–45:1.
Utimizo: Miaka 200 hivi baada ya unabii wa Isaya kutolewa, mfalme wa Uajemi alivamia Babiloni. Mfalme huyo aliitwa nani? Koreshi. Kwa kuwa jiji la Babiloni lilikuwa na kuta imara, Koreshi aliamua kugeuza mkondo wa Mto Efrati ambao ulipita kwenye jiji hilo. Wanajeshi wake walichimba mtaro ili kuelekeza maji ya mto huo upande mwingine. Hilo lilifanya kina cha maji kipungue kufikia kwenye magoti na hivyo jeshi la Koreshi liliweza kuvuka kwa urahisi mto huo ambao ulipita karibu na kuta za jiji. Kwa kushangaza, Wababiloni walikuwa wameacha malango ya jiji yaliyokuwa karibu na mto yakiwa wazi! Jeshi la Koreshi liliingia Babiloni kupitia malango hayo na kuliangusha jiji.
Hata hivyo, sehemu moja ya unabii ilibaki: Je, jiji la Babiloni liliacha kukaliwa? Watu waliendelea kuishi katika jiji hilo kwa karne kadhaa. Hata hivyo, leo, magofu ya Babiloni yaliyo karibu na jiji la Baghdad, nchini Iraq—yanathibitisha kwamba unabii huo ulitimia. Naam, Biblia inategemeka hata inapozungumzia matukio ya wakati ujao.
CHANZO KINACHOTEGEMEKA CHA KWELI
Hiyo ni mifano michache tu ambayo imewasaidia watu wengi kuona kwamba Biblia inatumainika, na si hilo tu ‘bali kama ilivyo kwa kweli, neno la Mungu.’—1 Wathesalonike 2:13.
Biblia ina mafundisho gani ya kweli? Je, mafundisho hayo yanaweza kukunufaisha? Makala zinazofuata zitazungumzia baadhi ya mafundisho ya msingi ya kweli za Biblia. Tutaanza kwa kuchunguza yale ambayo Biblia inafunua kuhusu mtungaji wake, yaani, Mungu.
Kiswahili Mapendezi
Copyright © 2019 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania Masharti ya Utumiaji Sera ya Faragha JW.ORG Ingia
